Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Yohana - Yohana 12

Yohana 12:34-46

Help us?
Click on verse(s) to share them!
34Mkutano wakamjibu, “Sisi tumesikia katika sheria ya kwamba Kristo atadumu hata milele. Nawe wasemaje, 'Mwana Adamu lazima ainuliwe juu'? Huyu Mwana wa Mtu ni nani?”
35Basi Yesu akawaambia, “Nuru ingalipo pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru, ili kwamba giza lisije likawaweza. Yeye aendaye gizani hajui aendako.
36Mngali mnayo nuru, iaminini nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Yesu aliyasema haya na kisha akaenda zake akajificha wasimwone.
37Ingawa Yesu alifanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, bado hawakumwamini
38ili litimie neno la nabii Isaya, alilosema: “Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”
39Ndio sababu wao hawakuamini, maana Isaya alisema tena,
40“Amewapofusha macho, na ameifanya migumu mioyo yao; wasije wakaona kwa macho yao na wakafahamu kwa mioyo yao, na wakaongoka nami nikawaponya.”
41Isaya alisema maneno hayo kwa kuwa aliuona utukufu wa Yesu na akanena habari zake.
42Walakini, hata wakuu wengi walimwamini Yesu; lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakukiri ili wasije wakatengwa na sinagogi.
43Walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
44Yesu akapaza sauti na kusema, “Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi tu bali na yeye aliyenituma mimi,
45naye anionaye mimi anamuona yeye aliyenituma.
46Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.

Read Yohana 12Yohana 12
Compare Yohana 12:34-46Yohana 12:34-46