Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 62

Zaburi 62:4-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
4Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. Selah
5Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
6Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
7Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
8Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. Selah
9Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
10Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
11Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.

Read Zaburi 62Zaburi 62
Compare Zaburi 62:4-11Zaburi 62:4-11