Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi

Zaburi 110

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
2Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
3Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
4Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
5Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
6Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
7Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.