1Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
2Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
3Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
4Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.