Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 88

Zaburi 88:3-9

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni.
4Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
5Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
6Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
7Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. Selah
8Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
9Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.

Read Zaburi 88Zaburi 88
Compare Zaburi 88:3-9Zaburi 88:3-9