Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 7

Zaburi 7:7-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Mataifa yote yamekuzunguka; uwatawale kutoka mbinguni.
8Yahweh, uwahukumu mataifa; uwaonyeshe kuwa sina hatia, Yahweh, kwa sababu mimi ni mwenye haki na sina hatia, Ewe uliye juu.
9Matendo ya waovu na yafike mwisho, bali uanzishe watu wenye haki, Mungu mwenye haki, wewe ambaye unapima mioyo na fahamu.
10Ngao yangu inatoka kwa Mungu, yule anaye okoa moyo wa mwenye haki.
11Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu anaye chukizwa na waovu kila siku.
12Ikiwa kuna mtu hatubu, Mungu atanoa upanga wake na ata andaa upinde wake kwa ajili ya vita.
13Ana jiandaa kutumia siraha kupambana naye; anatengeneza mishale yake kuwa ya moto.
14Fikiria kuhusu huyo ambaye ana ujauzito wa maovu, mwenye mimba ya mipango ya uharibifu, anaye zaa sumu ya uharibifu.
15Yeye huchimba shimo na kuliacha wazi kisha baadaye hudumbukia katika shimo alilochimba mwenyewe.
16Mipango yake mwenyewe ya uharibifu hugeukia kichwa chake mwenyewe, kwa kuwa vurugu zake mwenyewe humshukia kichwani pake.

Read Zaburi 7Zaburi 7
Compare Zaburi 7:7-16Zaburi 7:7-16