Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 77

Zaburi 77:2-10

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
3Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. Selah
4Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
5Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
6Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
7Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? Selah
10Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”

Read Zaburi 77Zaburi 77
Compare Zaburi 77:2-10Zaburi 77:2-10