16Ni nani atainuka kunitetea dhidi ya watendao uovu? Ni nani atasimama dhidi ya waovu kwa ajili yangu?
17Kama Yahwe asingelikuwa msaada wangu, haraka ningekuwa nimelala mahali pa ukimya.
18Niliposema, mguu wangu unateleza,” Uaminifu wa agano lako, Yahwe, uliniinua.
19Wasiwasi uwapo mwingi ndani yangu, faraja yako hunifurahisha.
20Kiti cha uharibifu chaweza kushirikiana nawe, kitungacho madhara kwa njia ya sheria?