Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 56

Zaburi 56:1-6

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
2Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
3Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
4Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
5Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
6Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.

Read Zaburi 56Zaburi 56
Compare Zaburi 56:1-6Zaburi 56:1-6