Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 50

Zaburi 50:1-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
2Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
3Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
4Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
5Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
6Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
7Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
8Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
15Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa

Read Zaburi 50Zaburi 50
Compare Zaburi 50:1-15Zaburi 50:1-15