2Vinywa vyetu vilijawa na vicheko na ndimi zetu zilijawa na kuimba. Kisha wakasema kati ya mataifa, “Yahwe amewatendea mambo makuu.”
3Yahwe alitufanyia mambo makuu; ni furaha gani tuliyokuwa nayo!
4Ee Yahwe, uwarejeshe mateka wetu, kama vijito vya kusini.
5Wale wapandao kwa machozi watavuna kwa kelele za furaha.
6Yeye aendaye akilia, akibeba mbegu kwa ajili a kupanda, atarudi tena kwa kelele za furaha, akileta miganda yake.