1Yahwe anatawala; nchi ishangilie; visiwa vingi na vifurahi.
2Mawingu na giza vyamzunguka. Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.
3Moto huenda mbele zake nao huwateketeza adui zake pande zote.
4Taa yake huangaza ulimwengu; nchi huona na kutetemeka.
5Milima huyeyuka kama nta mbele za Yahwe, Bwana wa dunia yote.
6Mbingu hutangaza haki yake, na mataifa yote huuona utukufu wake.