5Huwafagia kama vile kwa mafuliko nao hulala; na wakati wa asubuhi wako kama majani yameayo.
6Asubuhi yachipuka na kumea; jioni yakatika na kukauka.
7Hakika, tumeangamizwa kwa hasira yako, na gadhabu yako inatuogopesha sana.
8Umeudhihirisha uovu wetu mbele zako, na dhambi zetu zilizofichika katika nuru ya uwepo wako.