Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 86

Zaburi 86:1-8

Help us?
Click on verse(s) to share them!
1Sikia, Ee Yahwe, na unijibu, kwa kuwa ni maskini na mnyonge.
2Unilinde, maana mimi ni mwaminifu; Mungu wangu, umuokoe mtumishi wako anayekuamini.
3Unihurumie, Bwana, maana ninakulilia wewe mchana kutwa.
4Umfurahishe mtumishi wako, maana ni kwako, Bwana, ninaomba.
5Wewe, Bwana, ni mwema, na uko tayari kusamehe, na huonesha huruma kubwa kwa wale wanao kulilia wewe.
6Yahwe, sikiliza maombi yangu; sikia sauti ya ombi langu.
7Katika siku ya shida ninakuita wewe, kwa maana utanijibu.
8Katikati ya miungu hakuna wa kufananishwa na wewe, Bwana. Hakuna matendo kama matendo yako.

Read Zaburi 86Zaburi 86
Compare Zaburi 86:1-8Zaburi 86:1-8