Text copied!
Bibles in Swahili (individual language)

Zaburi 86:1-8 in Swahili (individual language)

Help us?

Zaburi 86:1-8 in Biblia ya Kiswahili

1 Sikia, Ee Yahwe, na unijibu, kwa kuwa ni maskini na mnyonge.
2 Unilinde, maana mimi ni mwaminifu; Mungu wangu, umuokoe mtumishi wako anayekuamini.
3 Unihurumie, Bwana, maana ninakulilia wewe mchana kutwa.
4 Umfurahishe mtumishi wako, maana ni kwako, Bwana, ninaomba.
5 Wewe, Bwana, ni mwema, na uko tayari kusamehe, na huonesha huruma kubwa kwa wale wanao kulilia wewe.
6 Yahwe, sikiliza maombi yangu; sikia sauti ya ombi langu.
7 Katika siku ya shida ninakuita wewe, kwa maana utanijibu.
8 Katikati ya miungu hakuna wa kufananishwa na wewe, Bwana. Hakuna matendo kama matendo yako.
Zaburi 86 in Biblia ya Kiswahili