11Usiniondoe uweponi mwako, na usimuondoe roho Mtakatifu ndani yangu.
12Unirudishie furaha ya wokovu wako, na unihifadhi mimi kwa roho ya utayari.
13Ndipo nitawafundisha wakosaji jia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
14Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
15Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
16Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
17Sadaka ya Mungu ni roho iliyovunjika. Wewe, Mungu hautadharau moyo uliopondeka na kujutia.