23Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
24Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
25Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
26Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.