1Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
2Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
3Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
4Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
5Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.