80Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
81Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
82Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
83Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
84Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
85Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
86Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
87karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.