1Oh njoni, tumwimbie Yahwe; na tumwimbie kwa shangwe mwamba wa wokovu wetu.
2Tuingie uweponi mwake kwa shukrani; tumwimbie yeye kwa zaburi ya sifa.
3Kwa maana Yahwe ni Mungu mkuu na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4Mkononi mwake zimo bonde za dunia; navyo vilele vya milima ni vyake.
5Bahari ni yake, maana aliiumba, na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.