36uzao wake utaendelea milele na kiti chake cha enzi kama vile jua mbele yangu.
37Kitaimarishwa milele kama mwezi, shahidi mwaminifu mawinguni.” Selah
38Lakini wewe umemtupa na kumkataa; umemkasirikia mfalme mpakwa mafuta wako.
39Wewe umelikataa agano la mtumishi wako. Umeinajisi taji yake ardhini.
40Umevunja kuta zake zote. Umeharibu ngome yake.
41Wapita njia wote wamemuibia, amekuwa kitu chenye kinyaa kwa majirani zake.
42Umeinua mkono wa kuume wa adui zake; umewafurahisha adui zake wote.