11Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
12Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
13Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
14Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.