1Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
2Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
3Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
4Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
5Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
6Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.