22Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
24Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
25Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
26Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
27Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.