Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 69

Zaburi 69:16-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
16Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
17Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
18Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
19Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
20Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
21Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.

Read Zaburi 69Zaburi 69
Compare Zaburi 69:16-22Zaburi 69:16-22