1Mpigieni Mungu kelele za shangwe, nchi yote;
2Imbeni utukufu wa jina lake; mzitukuze sifa zake.
3Mwambieni Mugu, “Matendo yako yanatisha kama nini! Kwa ukuu wa nguvu zako maadui zako watajisalimisha kwako.
4Nchi yote watakuabudu wewe na watakuimbia wewe; wataliimbia jina lako.” Selah