Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 50

Zaburi 50:8-14

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
9Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
10Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
11Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
12Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
14Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.

Read Zaburi 50Zaburi 50
Compare Zaburi 50:8-14Zaburi 50:8-14