13Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
14Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
15Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
16Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
17Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
18Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
19Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.