Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 22

Zaburi 22:15-22

Help us?
Click on verse(s) to share them!
15Nguvu zangu zimekaushwa kama kipande cha ufinyanzi; ulimi wangu unanata juu ya mdomo wangu. Wewe umenilaza mimi katika vumbi la mauti.
16Kwa maana mbwa wamenizunguka; kundi la watu waovu limenizunguka; wamenitoboa mikono yangu na miguu yangu.
17Nami ninaweza kuihesabu mifupa yangu. Wao wananitazama na kunishangaa.
18Wao wanagawa mavazi yangu kati yao wenyewe, wanapiga kura kwa ajili ya mavazi yangu.
19Usiwe mbali, Yahwe; tafadhali harakisha kunisaidia mimi, nguvu yangu!
20Uiokoe roho yangu na upanga, maisha yangu mwenyewe na makucha ya mbwa mwitu.
21Uniokoe na mdomo wa simba; uniokoe na mapembe ya ng'ombe wa porini.
22Nami nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu; katikati ya kusanyiko la watu nitakusifu wewe.

Read Zaburi 22Zaburi 22
Compare Zaburi 22:15-22Zaburi 22:15-22