Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 147

Zaburi 147:7-20

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Mwimbieni Yahwe kwa shukurani, mwimbieni sifa Mungu wetu kwa kinubi.
8Huzifunika mbingu kwa mawingu na huiandaa mvua kwa ajili ya nchi, akizifanya nyasi kukua juu ya milima.
9Huwapa wanyama chakula na wana kunguru waliapo.
10Hapati furaha katika nguvu ya farasi, wala haridhii miguu imara ya mwanadamu.
11Yahwe huridhia katika wale wanao muheshimu yeye, watumainio katika uaminifu wa agano lake.
12Msifuni Yahwe, Yerusalemu, msifuni Mungu wenu, Sayuni.
13Maana yeye huyakaza mapingo ya malango yako, huwabariki watoto wako kati yako.
14Huletamafanikio ndani ya mipaka yako, hukutosheleza kwa ngano bora.
15Huipeleka amri yake juu ya nchi, amri zake hupiga mbio sana.
16Huifanya theluji kama sufu, huitawanya barafu kama majivu.
17Hutupa mvua ya mawe kama makombo, ni nani awezaye kuhimili baridi aitumayo?
18Hutuma amri zake na kuziyeyusha, huvumisha upepo wake na hutiririsha maji.
19Hutangaza neno lake kwa Yakobo, amri zake na hukumu zake kwa Israeli.
20Hajafanya hivyo kwa taifa linginelo lolote, na kama ilivyo amri zake, hawazijui. Msifuni Yahwe.

Read Zaburi 147Zaburi 147
Compare Zaburi 147:7-20Zaburi 147:7-20