10Hapati furaha katika nguvu ya farasi, wala haridhii miguu imara ya mwanadamu.
11Yahwe huridhia katika wale wanao muheshimu yeye, watumainio katika uaminifu wa agano lake.
12Msifuni Yahwe, Yerusalemu, msifuni Mungu wenu, Sayuni.
13Maana yeye huyakaza mapingo ya malango yako, huwabariki watoto wako kati yako.
14Huletamafanikio ndani ya mipaka yako, hukutosheleza kwa ngano bora.
15Huipeleka amri yake juu ya nchi, amri zake hupiga mbio sana.