4Mtu ni kama pumzi, siku zake ni kama uvuli upitao.
5Ee Yahwe uziinamishe mbingu na ushuke chini, uiguse milima na uifanye kutoa moshi.
6Utume umeme uwatawanye adui zangu; upige mishale yako na uwavuruge.
7Nyosha mkono wako toka juu; uniokoe kutoka katika maji mengi, na kutoka katika mkono wa wageni.
8vinywa vyao hunena uongo, na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo.
9Nitakuimbia wimbo mpya, Mungu; kwa kinanda cha nyuzi kumi nitakuimbia sifa wewe,
10uwapaye wafalme wokovu, uliye muokoa Daudi mtumishi wako dhidi ya upanga wa uovu.