2Wao wanapanga uovu mioyoni mwao; wanasababisha mapigano kila siku.
3Ndimi zao zinajeruhi kama nyoka; sumu ya fira imo midomoni mwao. Selah
4Ee Yahwe, unilinde dhidi ya mikono ya waovu; unikinge na vurugu za watu wanaopanga kuniangusha.
5Wenye majivuno wameweka mtego kwa ajili yangu; wameeneza nyavu; wameweka kitanzi kwa ajili yangu. Selah
6Nilimwambia Yahwe, “Wewe ni Mungu wangu; usikie kilio changu unihurumie.”