8Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
12Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.