Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 135

Zaburi 135:2-11

Help us?
Click on verse(s) to share them!
2ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
3Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
4Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
5Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
6Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
7Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
8Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
9Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
10Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
11Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.

Read Zaburi 135Zaburi 135
Compare Zaburi 135:2-11Zaburi 135:2-11