5Maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, bali ni Yahwe aliye zifanya mbingu.
6Heshima na adhama ziko mbele zake. Nguvu na uzuri zimo katika patakatifu pake.
7Mpeni Yahwe sifa, enyi ukoo wa watu, mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
8Mpeni Yahwe utukufu ambao unastahili jina lake. Leteni matoleo na muingie nyuani mwake.