Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 92

Zaburi 92:3-15

Help us?
Click on verse(s) to share them!
3kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
4Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
5Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
6Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
7Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
8Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
9Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
10Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
11Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
12Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
13Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
14Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
15kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.

Read Zaburi 92Zaburi 92
Compare Zaburi 92:3-15Zaburi 92:3-15