9Wewe huitawala bahari yenye nguvu; mawimbi yainukapo, wewe huyatuliza.
10Ulimwangamiza Rahabu kama mmoja aliye uliwa. Uliwatawanya adui zako kwa mkono wako wenye nguvu.
11Mbingu ni zako wewe, na nchi pia. Uliiumba dunia na vyote vilivyomo.
12Uliumba kaskazini na kusini. Tabori na Hermoni hulifurahia jina lako.