Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 89

Zaburi 89:8-16

Help us?
Click on verse(s) to share them!
8Yahwe, Mungu wa majeshi, ni nani aliye na nguvu kama wewe, Yahwe? Kweli yako inakuzunguka.
9Wewe huitawala bahari yenye nguvu; mawimbi yainukapo, wewe huyatuliza.
10Ulimwangamiza Rahabu kama mmoja aliye uliwa. Uliwatawanya adui zako kwa mkono wako wenye nguvu.
11Mbingu ni zako wewe, na nchi pia. Uliiumba dunia na vyote vilivyomo.
12Uliumba kaskazini na kusini. Tabori na Hermoni hulifurahia jina lako.
13una mkono wa uweza na mkono wenye nguvu, na mkono wako wa kuume uko juu.
14Haki na hukumu ni msingi wa kiti chako. Uaminifu wa agano lako na uaminifu huja mbele zako.
15Wamebarikiwa watu wakuabuduo wewe! Yahwe, wanatembea katika nuru ya uso wako.
16Siku zote wanafurahia katika jina lako, na katika haki yako wanakutukuza wewe.

Read Zaburi 89Zaburi 89
Compare Zaburi 89:8-16Zaburi 89:8-16