4Umfurahishe mtumishi wako, maana ni kwako, Bwana, ninaomba.
5Wewe, Bwana, ni mwema, na uko tayari kusamehe, na huonesha huruma kubwa kwa wale wanao kulilia wewe.
6Yahwe, sikiliza maombi yangu; sikia sauti ya ombi langu.
7Katika siku ya shida ninakuita wewe, kwa maana utanijibu.