1Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
2Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. Selah
3Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
4Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.