13Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
14Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
15Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
16Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
17Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.