10Ngao yangu inatoka kwa Mungu, yule anaye okoa moyo wa mwenye haki.
11Mungu ni mwamuzi mwenye haki, Mungu anaye chukizwa na waovu kila siku.
12Ikiwa kuna mtu hatubu, Mungu atanoa upanga wake na ata andaa upinde wake kwa ajili ya vita.
13Ana jiandaa kutumia siraha kupambana naye; anatengeneza mishale yake kuwa ya moto.