Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:58-64

Help us?
Click on verse(s) to share them!
58Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
59Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
60Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
61Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
62Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
63Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
64Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:58-64Zaburi 78:58-64