Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:38-47

Help us?
Click on verse(s) to share them!
38Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
39Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
40Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
41Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
42Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
43alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
44Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
45Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
46Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
47Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:38-47Zaburi 78:38-47