Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 78

Zaburi 78:30-38

Help us?
Click on verse(s) to share them!
30Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
31Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
32Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
33Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
34Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
35Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
36Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
37Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
38Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.

Read Zaburi 78Zaburi 78
Compare Zaburi 78:30-38Zaburi 78:30-38