Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 77

Zaburi 77:7-13

Help us?
Click on verse(s) to share them!
7Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
8Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
9Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? Selah
10Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
11Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
12Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
13Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?

Read Zaburi 77Zaburi 77
Compare Zaburi 77:7-13Zaburi 77:7-13