16Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
17Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
18Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
19Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
20Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
21Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
22Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
23Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.