7Mwenye haki na astawi kwa wakati wake, na amani iwepo kwa wingi mpaka mwezi utakapotoweka.
8Na awe na mamlaka toka bahari na bahari, na kutoka Mto hadi miisho ya dunia.
9Na wote waishio jangwani wainame mbele zake; adui zake na walambe mavumbi.
10Wafalme wa Tashishi na visiwa walete kodi; wafalme wa Sheba na Seba watoe zawadi.
11Hakika wafalme wote wamwinamie yeye; mataifa yote yamtumikie yeye.
12Kwa kuwa yeye humsaidia mhitaji na maskini asiye na msaidizi.
13Yeye huwahurumia maskini na wahitaji, na huokoa maisha ya wahitaji.