Text copied!
CopyCompare
Biblia ya Kiswahili - Zaburi - Zaburi 69

Zaburi 69:21-29

Help us?
Click on verse(s) to share them!
21Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
22Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
23Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
24Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
25Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
26Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
27Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
28Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
29Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.

Read Zaburi 69Zaburi 69
Compare Zaburi 69:21-29Zaburi 69:21-29